Ufugaji wa kuku ni njia ya kuondokana na umasikini
WANANCHI mkoani Mkoa mpya wa Njombe wametakiwa kukataa umasikini kwa kubuni mbinu
mbalimbali ambazo zinaweza kuongeza vipato vya familia zao ikiwemo ufugaji wa
kuku.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa umoja wa wanawake wilaya ya Njombe katika mkoa mpya wa Njombe, Scholastika Kevela
wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani humo. Alisema kuwa, kila kaya ifuge
wastani wa kuku watano kwa ajili ya mikakati ya maendeleo kutokana na ukweli
kuwa bei ya kuku imeongezeka na kufikia Sh 10,000 kwa kuku moja.
Kevela alisema kuwa wakati sasa umefika kwa wananchi kuachana na
dhana kuwa wao ni masikini na badala yake kuwa wabunifu ili kuweza kujiletea
maendeleo kuanzia ngazi ya familia. “Wapeni kuku majina, ada, dawati, sare za
shule, maendeleo na mkitaka kuku wa kula mwambieni baba atafute kuku wa nyama
ndiye atakayechinjwa,” alisema kevela
Alisema kuwa, wananchi kama watafuga kuku na kuwauza kwa malengo
yaliyokusudiwa hawatakuwa na shida ya kupata ada kwa ajili ya kulipia karo za
watoto wao, kwani wana kuku wengi lakini hawana mipango ya jinsi kuku hao
watakavyoweza kuwasaidia pindi wanapouzwa.
Pia Bi.Kevela aliwataka
wananchi hao kupanda miti ili kuwezesha Mkoa wa Njombe kuwa wa kijani. Alisema
kuwa, kila nyumba iwe na miti mitano ikiwemo ya matunda ili kuweza kuhakikisha
upandaji wa miti unapewa kipaumbele. Alisema kuwa, kama wananchi watazingatia
kupanda miti na kuitunza basi kutakuwa na mabadiliko makubwa na Njombe itakuwa ya kijani.
Mwenyekiti huyo aliwataka viongozi wa dini kutumika kupaza
sauti za watoto kwa mara nyingi wanabeba uhalisia wa mambo yanayodhihirika kuwa
hawapati nafasi ya kusema.
No comments:
Post a Comment