Monday, May 28, 2012

MAENDELEO YA WILAYA YA NJOMBE
Na mwandishi wetu-Njombe

UWT yatoa masaada wa baiskeli
UMOJA wa Wanawake (UWT), Wilaya ya Njombe umetoa msaada wa baiskeli kwa wanawake wawili wenye ulemavu wilayani humo ambao pia ni wajane ili kuwasaidia katika harakati za maisha.

Msaada huo una thamani ya Sh1.5 milioni, ulitolewa na
Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Njombe, Scholastica Kevela katika Kata ya Mjimwema iliyopo Njombe Mjini.

Walemavu waliokabidhiwa baiskeli hizo ni Janeth Mfugale na Anna Mwagosela kutoka Kata za Igamba na Igominyi.

Akikabidhi msaada huo jana, Mwenyekiti wa UWT, Mkoa wa Iringa, Zainabu Mwamwindi alisema msadaa huo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2010/2015 ili kustawisha maisha ya watu wa makundi maalumu wakiwamo watu wenye ulemavu.

“Najisikia kuwa na furaha kubwa leo baada ya kuwakabidhi hawa wanawake baiskeli hizi maana maisha waliyokuwa wanaishi ni ya taabu sana kutokana na kutembea kwa kusota huku wakiwa na familia zinazowategemea,”alisema Mwamwindi.

Alisema UWT Mkoa wa Iringa inaipongeza UWT Wilaya ya Njombe kwa kuona umuhimu wa kuwasaidua wanawake hao na alimpongeza Mwenyekiti wa UWT wilaya hiyo kwa kutimiza ahadi ya kuwasaidia wanawake aliyoitoa alipokuwa anawania uongozi wa umoja huo.

Kwa upande wake Kevela alisema ni wajibu wa serikali na Watanzania wote
kuwasaidia watu wanaoishi katika mazingira magumu kama watu wenye ulemavu ili kujenga Tanzania yenye upendo, amani na mshikamano.

“Hawa kina mama na ni walemavu, lakini pia ni wajane, leo
najisikia furaha sana kwa kutoa msaada kwao maana niliwaona wakati nikiwa kwenye ziara zangu nikaahidi kuwasaidia ili kuwaondolea mateso waliokuwa wakipata,” alisema Kevela.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Mfugale alisema: “Najisikia vizuri sana leo, nimeishi kwa mateso kwa miaka mingi na hatimaye leo Mungu amesikia kilio changu, nawashukuru sana UWT Mkoa wa Iringa na hasa Mwenyekiti wetu wa Wilaya ya Njombe, kwa kuniondolea mateso haya.”

Naye Mwagosela alisema: “Sina ndugu nimekuwa naishi maisha magumu namshukuru sana Mungu na CCM kwa msaada huu, naomba waendelee na moyo huu.”

Diwani wa Kata ya Idamba, Chabiko Ihenga alisema msaada kwa wanawake hao
utaondoa simanzi na masikitiko yaliyokuwa yanatokana na maisha mgumu nay a tabu waliyokuwa wanaishi walemavu

No comments:

Post a Comment