Tuesday, May 29, 2012

                                                MSAADA WA HARAKA UNAHITAJIKA
       Mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa wanawake wilaya ya Njombe (UWT) Scholastika Kevela

Kutokana na mtoto wa kike katika mkoa mpya wa Njombe ameonekana kutumika sana kama YAYA katika mikoa mbalimbali ya Tanzania hususani katika jiji la Dar Es salaam na kunfanya mtoto huyo kuwa na mazingira magumu huku wakiishia kupata shida na kuhangaika huku wakikosa hata nauli ya kurudi makwao pindi wanapohitaji kufanya hivyo.

Watoto hao wamekuwa wakipata mimba za utotoni kutoka kwa baadhi ya waajiri wao huku wengine wakitafutiwa wanaume wakufanya nao ngono huku ujira akichukuwa mwajili wake  na yeye kuambulia maumivu na mateso ya kuingiliwa kinguvu bila lidhaa yake ukilinganisha na umri,na kuwasababishia matatizo ya kiafya huku wengine wakifikia hatua ya kupata maambukizi ya magonjwa ya zinaa na ugonjwa wa UKIMWI.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa jumuiya ya umoja wa wanawake wilaya ya Njombe (UWT) Silikcholastika Kevela alipokuwa akizungumza na wanahabari ofisini kwake huku akiitaka jamii kuacha tabia ya kuwakandamiza watoto hao na kuwataka wabadilike.

Kevela ameomba msaada wa wanajamii kujitolea katika kupambana na watu wanaoendelea kutoa ajira kwa watoto wadogo wa mkoa huo wakati wanayo nafasi ya kuendelea na masomo kwa mujibu wa fursa zilizopo za kielimu kwa sasa kutokana na sera ya elimu ya chama cha mapinduzi CCM chini ya mwenyekiti wake Dk.Jakaya Mrisho Kikwete.

Mwenyekiti huyo ameitaka jamii kuwakemea wazazi wanaokuwa na tamaa ya shilingi 20000 kwa mwezi ambayo bado haikidhi mahitaji ya mtoto huyo na badala yake kuishia kudhalilishwa kijinsia.

JE WATANZANIA TUFANYE NINI KUKABILIANA NA HILI ? kevela amesema maneno hayo akiashiria ni swali kwa jamii.

na McDonald Mollel Masse-Njombe

No comments:

Post a Comment