Tuesday, June 12, 2012

Tegete: Yanga imelamba dume kumsajili Yondani 


Tegete

 


MSHAMBULIAJI wa Yanga, Jerryson Tagete amesema kusajiliwa klabu hiyo ya Jangwani beki wa zamani wa Simba, Kelvin Yondan kutasaidia kufika mbali katika mashindano ya ndani na nje kutokana na uwezo mkubwa aliona mlinzi huyo.
Tegete aliyeongeza mkataba wa miaka miwili zaidi kuicheza Yanga, alisema ana imani kubwa na uwezo wa Yondani na kwamba uongozi wa Yanga hakufanya chaguo baya kumsajili.
 Mpachika mabao huyo wa Jangwani aliyepwaya msimu uliomalizika, amesema eye binafsi anafurahi kubaki Yanga na atakuwa tayari kuonyesha ushirikiano na beki wao mpya Yondani.
Akizungumza jana na kituo kimoja cha Radio, Tegete alisema kinachomfurahisha zaidi ni uwapo wa Yondani kwenye kikosi hicho kilichopoteza mwelekeo msimu uliopita na kumaliza ligi nafasi ya tatu ikiwa ni mara ya kwanza katika kipindi cha zaidi ya miaka 20.
"Tathimini yangu ni kwamba, Yondani ni beki mzuri anayekubalika na wengi. Kweli nafarijika kuja kwake Jangwani nikiamini atakuwa msaada mkubwa," alisema Tegete aliyewahi kuhusishwa kutaka kuhamia Simba msimu ujao.
Kuhusu kuongezewa mkataba, Tegete alisema amefurahishwa na hatua ya viongozi wake kwa vile ana mapenzi ya dhati na klabu hiyo ya Jangwani, mabingwa wa sas Kombe la Kagame.
"Sikuwahi kuwa na mpango wa kuhama Yanga, lakini naweza kufanya hivyo iwapo tu nitapata klabu ya kucheza nchi ya Tanzania na siyo kinyume chake," alisema.
Wakati huohuo, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amewataka viongozi wa Yanga na Simba kutoendelea na utamaduni wa kupoteza muda kwa mambo yaliyokosa mashiko.
Kauli hiyo ametoa jana baada ya kuwepo na mvutano kati ya viongozi wa timu hizo mbili juu ya usajili wa beki wa Simba Kevin Yondani ambaye inadaiwa kuwa amesajiliwa na Yanga.
Alisema viongozi wa timu hizo mbili wote wanazifahamu taratibu za usajili hivyo kama kuna udanganyifu kila kitu kipo wazi hivyo wasipoteza muda kwa mambo yasiyokuwa ya msingi.
"Lazima kati ya pende hizo mbili kutakuwepo na mmoja ambaye ni muongo hivyo hakuna haja ya kupoteza muda wa kupigizana kelele kwa sababu kila kitu kipo wazi" alisema Tenga.

No comments:

Post a Comment