Monday, June 18, 2012

MWAKALEBELA AKUNWA NA UJUMBE WA NAPE

 
NA mcdonald masse-Iringa
ALIYEKUWA mshindi wa kura za maoni ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) katika kinyang'anyiro cha kumsaka mgombea ubunge wa CCM jimbo la Iringa mjini mwaka 2010 Frederick Mwakalebela ameeleza kufurahishwa na kauli ya katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Taifa Nape Nnauye kuhusu ukweli wa mbunge Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA) kupita katika uchaguzi huo.

Hivyo awataka vijana wa kuacha kukimbilia vyama vya upinzani na badala yake kuendelea kutulia ndani ya CCM kwa madai kuwa kuna mikakati kambambe anayoifanya kwa ajili ya kuwawezesha vijana hao ili kuwa wajasiriamali badala ya kushinda vijiweni .
Alisema kuwa kuwa uwazi na ukweli wa Nape kuhusu makosa yaliyojitokeza katika jimbo hilo la Iringa mjini ni moja kati ya mambo ambayo wananchi wa jimbo la Iringa mjini walitegemea kuelezwa na kiongozi huyo .

Hivyo alisema kuwa mbali ya kuwa bado hajaamua kugombea ama kutogombea katika jimbo hilo ila bado ataendelea kuwa kada mzuri wa CCM na wala hatajaribu kukihama chama chake CCM kama ambavyo baadhi ya makada wenzake wanavyofanya.

" Napenda kumpongeza sana katibu wangu wa itikadi na uenezi Taifa Nape Nnauye kwa kuwaeleza ukweli wapiga kura wa jimbo la Iringa mjini ambao baadhi yao walikuwa wakirubuniwa na vyama vya upinzani kuwa labda CCM haitaweka ukweli wa kasoro zilizojitokeza katika uchaguzi mkuu mwaka 2010.....nataka vijana wa jimbo la Iringa mjini watambue kuwa mimi bado ni mwana CCM na nitaendelea kuwa karibu na chama changu"

Mwakalebela alitoa kauli hiyo leo alipozungumza na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kwa njia ya simu kuhusiana na msimamo wake kisiasa na maoni yake juu ya vijana wanaoendelea kushabikia upinzani kama njia ya kuchukizwa na hatua ya CCM mwaka 2010 kuengua jina la Mwakalebela.

Alisema kuwa ni vema vijana kutambua kuwa CCM ndicho chama chenye mwelekeo wa kuwatumikia wananchi na kuwa ni vema vijana hao kuendelea kubanana ndani ya CCM badala ya kuhama chama hicho.

Akielezea kuhusu mikakati yake ya kuwasaidia vijana wa jimbo hilo la Iringa mjini Mwakalebela alisema kuwa bado anauchungu na vijana wa Iringa mjini na hivyo amejipanga kuwasaidia kuwaunganisha na vikundi vya ujasiria mali pamoja na kuendelea kuwaunganisha vijana hao bila kujali itikadi ya kisiasa katika michezo ambayo itaanza hivi karibuni.

Kwa upande wake baadhi ya vijana na wazee wa mjini Iringa wamepongeza ziara hiyo ya Nape mjini Iringa kuwa ni ziara iliyolenga kumaliza uongo wa uongozi wa viongozi wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) dhidi ya serikali ya CCM .

Alisema mzee Ambweni Kyando mkazi wa Mwangata katika Manispaa ya Iringa kuwa bado anashangazwa na baadhi ya waliokuwa wagombea katuka kura za maoni ubunge jimbo la Iringa mjini akiwemo Zuberi Mwachura kukimbilia upinzani wakati ni mmoja kati ya makada wazuri wa CCM waliotegemewa kuja kupewa nafasi za juu

No comments:

Post a Comment