Monday, May 28, 2012

MWENYEKITI WA UWT NJOMBE KUKOMBOA WANAWAKE WA MKOA WA NJOMBE

Akizungumza na wanahabari wa mkoani humo mwenyekiti wa umoja huo Scholastika C.Kevela ameahidi kuwasaidia wanawake wa mkoa huo katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujasiliamali.

Amesema kutokana na mkoa huo kuwa na fursa nyingi za uwekezaji na kumilikiwa na wanaume pekee hivyo kuwafanya wanawake kuamini kuwa fursa hiyo ni kwa wanaume pekee huku akiita ni mtazamo hasi na badala yake wabadilike kwa kufanya kazi na kuthubuthubutu.

Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Njombe Scholastika Kevela (wa katikati) akizungumza na wanahabari wa mkoa mpya wa Njombe.

Picha na Mcdonald Mollel Masse-Njombe

No comments:

Post a Comment